Monday, October 19, 2015

MAHAFALI UROKI SEKONDARI TAREHE 17 OCTOBER 2015




MAHAFALI URKI SEKONDARI TAREHE 17 OCTOBER 2015

Siku hii ilithibitisha ule usemi wa Kiswahili kuwa siku njema huonekana asubuhi.



Wanafunzi wote walikua nadhifu na wenye haiba ya kisomi wengi wao wakiwa wamevalia sare mpya huku nyuso zao zikiakisi mwanga wa jua kwa tabasamu ambalo ni nadra sana kuliona shuleni na hasa shule za Tanzania. Hili lilikuwa jibu tosha kwa wale waliokuwa wakiuliza shule hii ina tofauti gani kubwa na shule nyingine? Mbona wazazi wengi wana watoto zaidi ya mmoja katika shule hii?

Baada ya ibada iliyoongozwa na mchungaji wa kituo (Chaplain) Mch Okuli Nkya, waafunzi na jumuiya nzima walikuwa na mapumziko mafupi ya kunywa chai nzito kwa wote.

Mapumziko yalimalizika baada ya nusu saa hivi na ndipo Maandamano ya kuingia ukumbinni yalipoanza kwa vishindo vya kwaito la nguvu.



Ndani ya ukumbi kelele za shangwe zilisikika kwa wale wanafunzi wangojezi ambao hawakuingia kwenye msafara huu, kelele zao zilikuwa kama kelele za maji mengi mfano wa yale ya maanguko ya maji ya Victoria kule Zimbabwe (Victoria Falls)



Mkuu wa shule Mwl Joseph Shahidi alionekana mwenye furaha  sana akitembea imara mithili ya askari tena wale wa mkoloni KAR, huku mkononi akiwa amebeba simu yake Smart Phone na bahasha yenye risala aliyomuandalia mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya ya Hai. 



Walimu na watumishi wengine nao walivalia vizuri sana. Jikoni muda wote kulikuwa na pilika pilika za kuandaa mahanjumati na kwa kuwa ukumbi haukua mbali sana na jikoni basi ungeweza kukisia aina za vyakula vilivyokuwa vinaandaliwa na hata kiasi cha mishikaki iliyokuwa imebanikwa jikoni.

Waandishi wa habari nao hawakuwa nyuma kuchukua matukio. Kwa kweli siku hii ilionekana ya kipekeee sana na yenye baraka zake nyingi sana.



Chapisho linalofuata litaelezea kinagaubaga ratiba nzima ya siku hiyo na tathmini ya wageni waliohudhuria. Hapa utweza kuona pia video na picha mnato nyingi kadri inavyowezeka.
Aidha kiamabatanisho cha risala zote na hotuba zote zilizotolewa siku hiyo zitajumuishwa.

Utapata nafasi ya kuwaona wahitimu wote na walimu baadhi waliokuwepo

Kwa sasa tuishie hapa

MAHAFALI UROKI SEKONDARI TAREHE


MAHAFALI UROKI SEKONDARI TAREHE 17 OCTOBER 2015

Siku hii ilithibitisha ule usemi wa Kiswahili kuwa siku njema huonekana asubuhi.

Wanafunzi wote walikua nadhifu na wenye haiba ya kisomi wengi wao wakiwa wamevalia sare mpya huku nyuso zao zikiakisi mwanga wa jua kwa tabasamu ambalo ni nadra sana kuliona shuleni na hasa shule za Tanzania. Hili lilikuwa jibu tosha kwa wale waliokuwa wakiuliza shule hii ina tofauti gani kubwa na shule nyingine? Mbona wazazi wengi wana watoto zaidi ya mmoja katika shule hii?

Baada ya ibada iliyoongozwa na mchungaji wa kituo (Chaplain) Mch Okuli Nkya, waafunzi na jumuiya nzima walikuwa na mapumziko mafupi ya kunywa chai nzito kwa wote.

Mapumziko yalimalizika baada ya nusu saa hivi na ndipo Maandamano ya kuingia ukumbinni yalipoanza kwa vishindo vya kwaito la nguvu.

Ndani ya ukumbi kelele za shangwe zilisikika kwa wale wanafunzi wangojezi ambao hawakuingia kwenye msafara huu, kelele zao zilikuwa kama kelele za maji mengi mfano wa yale ya maanguko ya maji ya Victoria kule Zimbabwe (Victoria Falls)

Mkuu wa shule Mwl Joseph Shahidi alionekana mwenye furaha  sana akitembea imara mithili ya askari tena wale wa mkoloni KAR, huku mkononi akiwa amebeba simu yake Smart Phone na bahasha yenye risala aliyomuandalia mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya ya Hai.




Walimu na watumishi wengine nao walivalia vizuri sana. Jikoni muda wote kulikuwa na pilika pilika za kuandaa mahanjumati na kwa kuwa ukumbi haukua mbali sana na jikoni basi ungeweza kukisia aina za vyakula vilivyokuwa vinaandaliwa na hata kiasi cha mishikaki iliyokuwa imebanikwa jikoni.

Waandishi wa habari nao hawakuwa nyuma kuchukua matukio. Kwa kweli siku hii ilionekana ya kipekeee sana na yenye baraka zake nyingi sana.




Chapisho linalofuata litaelezea kinagaubaga ratiba nzima ya siku hiyo na tathmini ya wageni waliohudhuria. Hapa utweza kuona pia video na picha mnato nyingi kadri inavyowezeka.
Aidha kiamabatanisho cha risala zote na hotuba zote zilizotolewa siku hiyo zitajumuishwa.

Utapata nafasi ya kuwaona wahitimu wote na walimu baadhi waliokuwepo

Kwa sasa tuishie hapa











MAHAFALI KIDATO CHA NNE 2015
Siku ilianza kwa Bashasha na msisimuko mkubwa sana.
Wanafunzi wakiwa wamevalia Sare zao safi zilizolandanda kabisa na haiba ya uanafunzi miongoni mwazo zikiwa mpya toka dukani huku zikinukia marashi ya kupendeza, waliianza siku kwa shukrani kwa Muumba wao katika ibada iliyoongozwa na Mchungaji wa Shule (Chaplain) Rev Okuli Nkya.

Ilipofika muda wa saa tatu hivi, wanafunzi na watumishi walijumuika kwa Chai nzuri ili kukoleza furaha ya siku.

Mara baada ya chai ndipo shangwe na nderemo zilipovumva ukumbini mfano wa maanguko ya maji kule Victoria (Victoria Falls) kule Zimbabwe zikipambwa na nyimbo na miruko ya Kwaito. Kidato cha nne walijipanda msururu mrefu uliomeremeta na huku wakicheza kwaito kwa nguvu zao zote wakiingia kwa maandamano ukumbini. Kwa nyuma watumishi na wageni wote walijiunga kwa mbwembwe na makofi.



Mkuu wa shule Mwl Joseph Shahidi alikuwa muda wote akitabasamu na mkononi akibeba bahasha yenye risala aliyomwandalia mgeni Rasmi. Miongoni mwa wageni waliokuwako ni Mzazi rasmi Mwl Philipo Kiula na wajumbe kadhaa wa Bodi ya shule.

Katika mada zitakazofuata tutaambatanisha video na nyimbo mbali mbali zilizoipamba siku hiyo

Sunday, February 8, 2009

Uroki On the Internet

Uroki school has started its blog where it will be able to share news with friends. This Blog was created by Ben our AIESEC friend